SIKU chache baada ya ndoa ya mwigizaji, Ndubagwe Mithayo ‘Thea’ kuvunjika, mwigizaji Deogratius Shija ‘Shija’ ameibuka na kueleza maumivu anayoyapata juu ya tukio hilo.
“Ndoa siyo maigizo. Ndoa ni mkataba mkubwa sana ambao wanaingia wanadamu hivyo inapovunjika huwa haileti picha nzuri kwa Mungu, binafsi inaniuma sana,” alisema Shija.






