HIVI NDIO VITU AMBAVYO UKIVIFANYA BASI MWANAMKE WAKO HATA KUACHA

Hili limekuwa kama ni fumbo gumu kwa baadhi ya wanaume.Leo nimeonelea kuileta hii mada kwenu wapenzi wa hii blog ni vitu vipi vinavyomvutia zaidi mwanamke hasa kwa mwanaume.Mwanamke atavutiwa kwako endapo utamfanyia yafuatayo:


KUMSIFIA
Wanaume wengi hupuuzia hili, huona kama ni jambo lisilo na maana sana kwao na wenzi wao. Hali ni tofauti sana kwa wanawake ambao hupenda kuwasifia wanaume zao. Nitakupa mifano miwili ya namna wanandoa wa jinsia mbili tofauti wanavyotambulishana kwa jamaa zao.
MWANAUME: “Peter kutana na mke wangu, anaitwa mama Diana. Nipo naye mwaka wa tatu sasa, tuna watoto wawili, huyo Diana na mwingine anaitwa Cris. Mama Diana, huyu ni Peter nilisoma naye A – Level, Tosamaganga Sekondari.”
MWANAMKE: “Suzan, huyu ndiye mume wangu mpenzi...anaitwa Elifaraja lakini mimi napenda zaidi kumuita Elly. Kiukweli nampenda sana mume wangu jamani, tuna mtoto wetu mmoja, anaitwa Agness. (Akimgeukia mumewe) Baby, huyu hapa ni rafiki yangu Suzan. Yaani tumekua naye mtaa mmoja huko Arusha.”

ANGALIA TOFAUTI
Bila shaka kwa namna wawili hao walivyotambulishana unaweza kuona tofauti kubwa. Mwanaume amemtambulisha mkewe kawaida kabisa, hajaonesha manjonjo au namna anavyompenda na kumthamini mwenzake, lakini mwanamke amefanya hivyo.
Sikia nikuambie, KUMSIFIA mwanamke, kuna nafasi kubwa sana kwake. Chunguza kwa makini, hata kunapokuwa na mgongano katika familia, halafu wakatokea wageni, baada ya utambulisho na mazungumzo ya hapa na pale, wageni wakiondoka kunakuwa na uwezekano mkubwa zaidi wa kumaliza mpasuko katika familia.
Jenga utamaduni wa kumsifia mpenzi wako, unamuweka katika kilele cha upendo. Anajiona kamili, peke yake na mwenye nguvu kwako. Anajiamini na unamfanya azidi kukupenda kwa kuwa anaamini yupo na mwanaume ambaye anajivunia kuwa naye. 

MALENGO
Wanaume wengi wana ulemavu mmoja; hawapendi kuwashirikisha wanawake katika mambo yao. Wanapenda kufanya mambo yao kwa siri na wakati mwingine ikilazimika kumwambia mkewe basi kwa mshtukizo baada ya kukamilisha jambo husika.
Hii si sahihi. Dunia ya leo imebadilika rafiki zangu. Inawezekana wazee wa zamani walikuwa sahihi, maana ilikuwa ni suala la kununua ng’ombe na kuwaweka katika zizi kwenye kijiji cha jirani, halafu wanapewa malisho mazuri, baada ya miaka miwili wanazaliana, hapo ndipo anamweleza mkewe.
Siku hizi dunia imebadilika, kuna mambo mengi. Kuna suala la hasara katika biashara, utapeli n.k. Mkeo ndiye rafiki yako mkubwa kuliko wote, ndiye ndugu yako wa karibu zaidi kuliko yeyote. Yes! Mkeo ndiye ndugu yako maana umetengeneza naye familia. Mmeshirikiana kuzaa watoto na kujenga maisha pamoja.
Yeye anapaswa kujua mambo yako, ndiye mtetezi wako nambari wani. Mweleze juu ya malengo yako, wakati mwingine anaweza kukusaidia sehemu ambayo hukutarajia.
Hata hivyo, kumshirikisha katika malengo yako, kunampa nguvu na nafasi ya kujiona mama katika familia yenu. Msaidizi kamili wa nyumba yenu.

KIPAUMBELE
Kuna wakati wanawake huwa na mambo yao binafsi. Kazini au kifamilia. Inawezekana akatatizika katika eneo fulani ambalo kwa namna moja ama nyingine atahitaji usaidizi wako. Ikitokea mkeo akawa katika hali hiyo, msikilize.
Mathalani ana tatizo la kifamilia, amekuambia mmoja wa wazazi wake anaumwa, msaidie. Si lazima kifedha, lakini kuonesha kujali kwako tu, kutampa matumani kwamba anaishi na mtu sahihi. Acha kupuuza mambo yake; hata yale madogo, kama ya ‘mtoto wa dada amerudishwa ada shuleni’.
Msikilize, mshauri panapofaa kufanya hivyo na ukiweza msaidie hata kifedha. Katika upande wa pili ni hivyo hivyo. Labda una tatizo binafsi, kazini kwako au kifamilia, mshirikishe.
Unaweza kushangaa jambo ambalo uliamini unaweza kulimaliza peke yako, kwa  kumshirikisha likawa jepesi zaidi na mambo yakaendelea vyema. Kipaumbele kwa namna yoyote ile, kunaongeza mapenzi zaidi kwa mwanamke.

TENDO LA NDOA
Hiki ni kipengele nyeti, kinachohitaji lugha nzuri ya kirafiki kukifafanua. Hakuna siri, tendo la ndoa ni moja ya kiwakilishi cha ndoa. Maana hata maandiko yanasema: “Mwanamke ataacha wazazi wake na kwenda kwa mumewe, nao watakuwa mwili mmoja.”
Kimsingi tendo la ndoa lina nafasi yake. Ni muhimu likaheshimiwa na kutengewa muda maalum wa kufurahia. Si papara. Kwa bahati mbaya wanaume huwa si wafuatiliaji sana wa kujua namna ya kuwafurahisha zaidi wenzao. Wenyewe wanajiwazia wenyewe. Wanafikiria namna ya kuwakomoa wenzao.
Si sahihi. Tendo la ndoa halina maana ya kukomoana. Jenga mazoea ya kufanya maandalizi kamili kabla ya tendo. Sikiliza hisia za mwenzako. Ukiweza kumjulia mke wako katika eneo hili, ni wazi kwamba utazidisha upendo wake kwako, lakini pia atakuwa katika kuta za uaminifu. Akatafute nini nje wakati wewe ndiye mganga wake unayeweza kumtibu barabara?
Kuna kitu nimesahau kweli? Kama kipo nitafute pembeni, kwa hapa haya yatoshe kukufanya uelewe nilichotaka kukuelekeza. Nikuache na neno moja; uamuzi wa kuijenga ndoa yako upo mikononi mwako. Ukitaka iwe shaghalabaghala, pia ni wewe tu! Ahsante kwa kunisoma.

LAANA: MWANAMKE ALIYEFANYA MAPENZI NA DOLPHIN AFUNGUKA MANENO MAZITO, YASOME HAPA

mager
Unaweza kushangaa na kuona ni kitu cha ajabu lakini hii imetokea ambapo mwanamke ambaye alifanya mapenzi na samaki aina ya Dolphin ikiwa ni sehemu ya utafiti wa kisayansi amezungumza kwa mara ya kwanza juu ya hatua hiyo.
Mwanamke huyo Margaret Howe Lovatt ambaye ni mtafiti wa wanyama amesema alikuwa sehemu ya utafiti huo uliofanyika katika kisiwa cha Virgin nchini Marekani kwa ajili ya kuwafundisha viumbe wa baharini wenye akili jinsi ya kuongea kiingereza.
Margaret Lovatt Howe
Margaret Howe Lovatt anasema alikuwa akijaribu kumfundisha Peter (the dolphin) jinsi ya kuongea kiingereza lakini uhusiano wao ulikwenda mbali zaidi.
Ilikuwa mnano wa mwaka 1963 ambapo walimsaidia kutengeneza bwawa la Dolphin nyumbani kwake ambako wanasayansi wangeweza kuwasoma wanyama hao wakiwa nyumbani, ndipo hapo Margaret alipokuna na Peter ambaye ni samaki aina ya Dolphin kwa wakati huo akiwa bado mdogo ambapo wawili hao wakapatana na mahusiano yao kukua zaidi kimwili.
Margaret amenukuliwa akisema kuwa “Peter (Dolphin) alipenda kuwa na mimi, mara nyingi alikuwa akijisogeza mwenyewe karibu yangu kwenye mguu wangu au mkono na kuruhusu kitendo hicho.”
dolphin
Anaendelea kusema kuwa “Haikuwa shida kwangu kwani Peter alikuwa akihisi uwepo wangu na kuona ni kitendo cha kimapenzi kwa upande wake lakini kwangu niliona ni kitu cha kawaida kama sehemu ya masomo yangu.”

MAHUSIANO: MAPENZI KIPINDI CHA UJAUZITO

Leo naomba kuleta maada hii mezani baada ya mabishano mengi na maswali mengi kutika kwa wadau wangu Nimefikia hatua mara baada ya
mabishano na mijadala kadhaa ya watu wazima kuhusu mapenzi, staili na madhara kipindi cha ujauzito! kwa leo mimi ntasema machache nnaimani mengi yanajulikana tayari.
                  Kabla yote ieleweke kwamba wapo baadhi ya wanawake ambao inapofika kipindi cha Ujauzito huwa hawapendi hata kuguswa bega na waume zao, kama hali ikiwa hivi, mume usimmaind sana, elewa ni mapito tu na "atarudi kundini soon" Pia wapo baadhi ya wanawake ambao wanapokuwa na ujauzito basi hamu ya kufanya mapenzi huongezeka maradufu na inawezekana wakataka "Uroda" Kila siku, hapo pia mzee mwezangu jua ni mapito, yataisha tuu! Kikubwa ni kuelewa Mkeo yupo katika hali gani na kujitahidi kadri ya uwezo wako kwenda nayo sawa.
            
Mbali na hayo napenda niseme kuwa "INAWEZAEKANA" kabisa Mume na Mke Kufanya mapenzi kipindi cha Ujauzito wa Mke mpaka siku anayojifungua, bila kuhofia eti utamjeruhi mtoto maana kabla haujafikia alipo mtoto kuna Matabaka ambayo yanamkinga mtoto na uvamizi wa nje hasa wa "Dudu" ya Baba!
Kuhusu Staili nakuomba mume usiwe unampinda sana Mkeo maana utakuwa unamuumiza tumbo, piga zile za kale tu! Pia Kama Mke unawasiwasi na Hali yako ni vizuri ukamwona Daktari wako wa Kliniki kwa maelezo au vipimo vya ziada!

USHIRIKINA: MWISHO WA DUNIA UMEKARIBIA..!! FREEMASON WATOA TAMKO KUHUSU MWISHO WA DUNIA HII..!!

WAKATI binadamu wakiendelea na mipango yao ya kuifanya dunia kuwa sehemu salama ya kuishi kimazingira, kiulinzi na usalama, utabiri mpya wa kutisha unaonesha kuwa mwaka 2032 ndiyo mwisho wa sayari hii ya tatu katika mfumo wa jua. Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali katika mitandao ya internet,
sayari iitwayo Nibiru, ambayo kisayansi inafahamika kama Planet X ipo njiani kuigonga dunia na hivyo kusababisha majanga mbalimbali kutokea. ITAONEKANA ANGANI KAMA MWEZI
Kwa mujibu wa mitandao hiyo ya kisayansi, sayari hiyo ambayo inaisogelea dunia kwa kasi kubwa, itaonekana kubwa na angavu wakati wa usiku angani na kuwa katika umbo la mwezi na hivyo kufanya miezi ionekane miwili.
 DALILI KWAMBA IPO JIRANI
Taarifa zaidi za kisayansi zinasema kuwa, kadiri sayari hiyo inavyozidi kusogea, dunia itaanza kutikisika na kusababisha matetemeko ya ardhi kuongezeka sehemu mbalimbali.
 Mbali na dunia kutikisika na matetemeko, milipuko ya volcano nayo itatokea huku idadi kubwa ya milipuko hiyo mipya ikiongezeka, vimbunga vikubwa kama Tsunami vitaibuka na mwishowe dunia itapigwa na bomu la miamba midogo na vimondo kutokea angani. DUNIA ITAKUMBWA NA GIZA NENE
Wakati volcano zote duniani zitakapoanza kulipuka na zingine mpya kujitokeza, dunia itafunikwa na giza nene  na matope kwa wakati wote wa usiku na mchana huku watu wakitakiwa kusoma katika Biblia Joel 2: 1-2 na Zephaniah 1:14-17.
 NI TUKIO LA AINA YAKE KARNE YA 21
Nibiru inatajwa kama kitu kinachoisogelea dunia kinachoaminiwa kusababisha madhara makubwa ambapo kama hakitaigonga dunia, kitasababisha mtikisiko usio wa kawaida kitakapopishana nayo. Baadhi ya wanasayansi wanaamini kuwa kitendo hicho kitatokea mapema katika karne ya 21 (tuliyonayo sasa).
 WANASAYANSI WAPINGANA
Baadhi ya wanasayansi wanapinga kwa maelezo kwamba hakuna ushahidi wowote wa kitafiti unaoonesha wazi kwa mabingwa wa anga za juu waliobobea wa masuala ya nyota.
 MWANAMKE ALIWAHI KUOTA NDOTO
Kwa mara ya kwanza jambo hilo lilitokea mwaka 1995, wakati mwanamama Nancy Lieder muasisi wa mtandao wa ZetaTalk, aliwahi kudai kuoteshwa ndoto kwamba, Mei 2003 kuna kitu kitaingilia mfumo wa jua (solar system) na kusababisha dunia kutoboka tundu litakalosambaratisha sehemu kubwa ya kizazi cha binadamu.
 Lieder aliifafanua kuwa, kitu hicho kitakuwa na ukubwa wa mara nne ya dunia. BAADA YA NDOTO
Baada ya mwanamama Lieder, mtu wa kwanza kuizungumzia Nibiru alikuwa Mark Hazlewood, mwanachama wa zamani wa mtandao wa ZetaTalk ambaye mwaka 2001 alichapisha kitabu kilichoitwa Blindsided na kusema kuwa mwisho wa dunia ungekuwa mwaka 2003 baada ya kuwasili kwa sayari ya kumi (Nibiru).
 Katika mfumo wa sasa, baadhi ya wanasayansi wanasema sayari ziko 12, wakizitaja kwa namba 1. Jua 2. Mercury 3. Venus 4. Dunia 5. Luna (mwezi) 6. Mars 7. Jupiter 8. Saturn 9. Uranus 10. Neptune 11. Pluto 12. Nibiru. IMANI NYINGINE YASEMA MWISHO WA DUNIA NI FEBRUARI 22, 2014
Hata hivyo, utabiri mpya uliotolewa na watu wa jamii ya Vikings jijini New York, Marekani umesema mwisho wa dunia ni Februari 22, mwaka huu.
 Mitandao mbalimbali pamoja na gazeti maarufu la Daily Mail la Uingereza lilielezea utabiri huo uliofanywa na jamii hiyo ukidai kuwa mwisho wa dunia utatokana na Mungu Odin kupigana na kuuawa na shetani Wolf Fenrir, hivyo kuiachia dunia anayoishikilia.Wamesema baada ya kuiachia dunia itafurika maji ambayo yatakuwa na sumu, hivyo viumbe wote watateketea. WATUMISHI WA MUNGU TANZANIA
Baadhi ya watumishi wa Mungu nchini wamekuwa wakisimamia andiko la kwenye Biblia linalosema kuwa, hakuna mwanadamu anayeijua siku wala tarehe ya mwisho wa dunia na ni siri ya Muumba.
 Makanisa mengi nchini Tanzania yana sera tofauti lakini yanaongozwa na Biblia moja. Makanisa hayo ni Romani Katoliki, Lutheran (KKKT), Anglikana na makanisa ya kiroho kama Full Gospel& Bible Fellowship la Zakaria Kakobe. FREEMASON WABARIKI
Jamii ya Freemason tayari imebariki mwisho wa dunia kwamba umefika na dunia inatarajie tukio kubwa la pamoja.
 Mitandao ya jamii hiyo inataja kama hizi ni nyakati za mavuno kwa maana kwamba, upande wa Mungu na shetani kushindania watu huku waendao upotevuni  wakiwa wengi. MFUMO WA DUNIA TANGU KUUMBWA
Kwa mujibu wa kitabu kinachoitwa Panorama ya Biblia, ulimwengu tangu kuumbwa kwake umekuwa na matukio makubwa kila baada ya miaka 2000 (inaweza isitimie au ikapita kidogo).
 Tangu kuumbwa kwa Adamu na Eva mpaka gharika inadaiwa ni miaka 2000. Gharika hadi dunia kubadili mfumo wa mawasiliano (Mnara wa Babeli) ni miaka 2000. Kuzaliwa kwa Yesu hadi saa ni miaka 2000 ambapo katika karne hii, dunia huenda ikaingia katika tukio kubwa sana ambalo halijawahi kutokea

DADA YAKE DIAMOND PLATNUMZ "ESMA" NA PETIT MAN WAKUACHE, PICHA HIZI HAPA WAKIDENDEKA

  Ni habri mpya ya mjini kwa sasa,ndoa ya Dada wa Diamond na kipenzi wa Wema petiti man wakuache,amabapo uhusiano wao ulioanza kama utani hatimae  umezalisha kile amabcho wengi hawakukitgemea kama kingekuwa mapema hivi...Tunawatakia maisha mema ya ndoa na barka tele

MSANII BONGO FLEVA ANASWA NA MA-MISS WAKIPIGA PICHA ZA UTUPU HUKU AKIWACHEZEA SEHEMU NYETI, SOMA HABARI HII HAPA

Msanii wa kitambo wa Bongo Fleva aliyewahi kutamba na Kundi la Chamber Squad na ngoma yake ya taifa ya Kama Vipi, Moses Bushagama ‘Mez B’ anadaiwa kuwaaibisha ma-miss kwa kuwalazimisha kupiga nao picha wakiwa watupu.
Msanii wa kitambo wa Bongo Fleva wa Chamber Squad Moses Bushagama, ‘Mez B’ akijiachia na 'totoz' fukweni.
Tukio hilo la kidhalilishaji na lisilovumilika lilijiri juzikati kwenye Ufukwe wa Mikadi uliopo Kigamboni jijini Dar muda mfupi baada ya jamaa huyo ‘kushuti’ video ya ngoma yake mpya ya Shemeji.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, jamaa huyo aliwafuata warembo hao waliojitambulisha kwa majina ya Vicky na Rebecca waliokuwa kwenye swimming pool (bwawa la kuogelea) ambao ilisemekana kuwa siyo raia wa Bongo na huko wanakotokea ni ma-miss.
Ilidaiwa kwamba Mez B ndiye aliyewaomba kupiga nao picha lakini jamaa huyo ‘akaharibu’ baada ya kwenda mbele zaidi na kuanza kuwaminya ‘vifuu’ vyao kifuani vilivyoonekana ni vya saa sita vilivyokuwa wazi bila hata ‘braa’.
Mmoja wa ma-miss hao akiwa mtupu sehemu kubwa tu ya mwili wake.
Ilisemekana kwamba baada ya kupiga picha hizo, yeye (Mez B) aliwafowadia washikaji zake ndipo zikazagaa kupitia mtandao wa WhatsApp.
“Hawa wasanii wetu kweli ni majanga. Ona Mez B alichokifanya na hawa mabinti. Yaani wapo kama walivyozaliwa lakini yeye yupo freshi na nguo zake. Kama siyo kudhalilishana ni nini! Amewaaibisha sana. Lakini na wao hawakuona?” alihoji mrembo mmoja aliyefowadiwa  picha hizo na rafiki yake kwenye WhatsApp.
Baada ya kuzitia picha hizo kibindoni, gazeti hili lilimtafuta Mez B kisha kumbana kuhusu tukio hilo ambapo alijitetea kwa ufupi:“Wale ma-miss walikuwa wanaogelea vifua wazi kwa muda mrefu. Wao ndiyo walioniomba kupiga nao picha.”
Kumekuwa na kasumba ya kupiga picha za utupu kisha kuziachia mtandaoni kwa kudhani kuwa ni kujiongezea umaarufu lakini ukweli ni kujiondolea utu na heshima mbele ya jamii.

ANT EZEKIEL AENDELEZA UMALAYA WAKE, WANASWA AKIWA KIMAHABA NA KASSIM NCHINI MAREKANI

Wakati mumewe Sunday Demonte akidaiwa kuwa yuko mbioni kuhukumiwa kwenda jela huko Dubai, staa wa Bongo Movies, Aunt Ezekiel Grayson amenaswa laivu kimahaba nchini Marekani akiwa na msanii wa muziki wa Kizazi Kipya, Kassim Mganga.
Staa wa Bongo Movies, Aunt Ezekiel Grayson amenaswa laivu kimahaba nchini Marekani akiwa na msanii wa muziki wa Kizazi Kipya, Kassim Mganga.
Wakati anaondoka nchini hivi karibuni, Aunt alionekana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar, akiwa na mwanaume ambaye anadaiwa kuwa ni mume wa mtu, Moses Iyobo ‘Moze’.Baada ya habari hiyo kuripotiwa na gazeti tumbo moja na hili, Ijumaa Wikienda, Septemba 15, mwaka huu, ilidaiwa kwamba ndugu wa mumewe, Sunday hawakufurahishwa na kitendo hicho.
Wakipata msosi.
“Tunashangaa kumuona Aunt ameambatana na mume wa mtu na huko anakoenda pia tunasikia watakuwa wawili tu na Kassim, inatutia shaka kwa kweli,” alisema mmoja wa ndugu wa mume kwa sharti la kutoanika jina lake.
Kwa mujibu wa chanzo chetu kilichopo nchini Marekani, wawili hao walitia maguu hivi karibuni kwa mwaliko maalum wa Ubalozi wa Tanzania nchini humo ambapo Kassim alipewa nafasi mbili hivyo akaamua kumchukua Aunt.
Msanii wa muziki wa Kizazi Kipya, Kassim Mganga.
“Kassim aliambiwa atafute kampani ya kuja nayo huku ndipo akaona Aunt anafaa kwa kuwa mwenyewe amedai ni mtu wake wa karibu,” kilisema chanzo hicho.
Chanzo hicho kilizidi kumwaga data kwamba, baada ya wawili hao kufika nchini humo, walipanga katika hoteli moja kisha kuanza kujiachia kwenye viwanja tofautitofauti wakila bata ndani ya Jiji la New York.
Staa wa Bongo Movies, Aunt Ezekiel Grayson.
Baada ya mwanahabari wetu kunasa mchapo huo, alimtafuta Aunt kupitia WhatsApp hakupatikana, bahati nzuri Kassim alipatikana na kusema:“Tumekuja kwa mwaliko wa ubalozi wetu, Aunt ni mshkaji wangu kwa hiyo usishangae sana nikila naye bata,” alijibu Kassim.

MTOTO WA MCHUNGAJI, MWANAKWYA KANISANI AKIWA NA MTOTO MGONGONI WANASWAKICHAKANI

Wanakwaya wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God, Hanipher na Godfrey (mtoto wa mchungaji) walionaswa wakiwa kichakani.
Hivi karibuni mjini Iringa, wanakwaya wawili wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God, mwanamke alijitambulisha kwa jina moja la Hanipher na mwanaume aliyesema anaitwa Godfrey, walinaswa usiku kichakani katika mazingira yaliyojaa utata, Risasi Jumamosi linakupa kisa kamili.
NI MAKABURINI
Tukio hilo la kushangaza, lilijiri kwenye eneo la Makanyagio ambalo lina makaburi ya awali katika Manispaa ya Iringa licha ya kuwepo na nyumba za wenyeji pia.

KAZI YA SUNGUSUNGU
Kwa mujibu wa chanzo chetu, wanakwaya hao walinaswa na sungusungu ambao siku za hivi karibuni wamekuwa wakifanya ‘patroo’ katika eneo hilo na la Isoka kufuatia kuwepo kwa matukio ya wakazi wake kuvamiwa, kupigwa na kuporwa mali.

SIKU YA TUKIO
Siku ya tukio, sungusungu  hao wakiwa katika majukumu yao  waliwaona  wanakwaya hao wakiacha njia kuu na kuchepukia porini umbali unaokadiriwa kuwa mita 20 kutoka barabarani.

“Ilibidi sungusungu wawafuate hadi kule kichakani, ndipo walipowakuta katika mazingira tata na yenye maswali mengi bila majibu. Mbaya zaidi, yule mwanamke alikuwa na mtoto wa mwaka mmoja mgongoni,” kilisema chanzo chetu.
Wanakwaya wakifunguka kueleza kisa cha kuwa kichakani usiku mnene.
WAPEWA KICHAPO, WAJIANIKA
Chanzo kikadai kuwa, sungusungu hao waliwapa kichapo chepesi ili waweze kusema walikuwa wakifanya nini na wao ni akina nani, ndipo mwanamke huyo akaweka wazi mambo kwamba, yeye ni mkazi wa Kitongoji cha Isoka ilhali kijana huyo ni mwimbaji mwenzake wa kwaya lakini pia ni mtoto wa mchungaji wa kanisa hilo.

ETI?
Katika hali ya kushangaza, mtoto huyo wa mchungaji huku akiomba samahani kwa kunaswa kichakani, alisema eti kilichowapeleka huko muda huo wa usiku ni kumsaidia mwanamke huyo kumwingizia nyimbo za dini kwenye simu yake!!

AKIRI SI MWENENDO MWEMA
Pamoja na yote, Godfrey  alikiri kuwa kitendo cha kuingia kichakani na mwanamke muda huo wa saa 2.15  usiku kilikuwa ni hatari kwao kiimani na hata usalama wa miili yao kwa ujumla.

Kiimani alikuwa na maana kwamba, kuonekana kichakani watu waliookoka hakutoi picha nzuri kwa jamii inayotakiwa kuhubiriwa ili watu wamrudie Mungu, usalama wa miili ni kama vile kuumwa na nyoka au wadudu wengine wenye kudhuru.
SUNGUSUNGU NAYE
Akizungumza na Risasi Jumamosi, mmoja wa sungusungu hao alisema haikuwa rahisi kwao kuamini kwamba wawili hao waliingia kichakani kuingiziana nyimbo kwenye simu.

“Hivi kweli mtoke barabarani muingie kichakani kisa kuwekeana nyimbo kwenye simu, inaingia akilini kweli? Labda bwana,” alisema sungusungu huyo bila kutaja jina lake akidai wana bosi wao ndiye alitakiwa kusema. Baada ya kuwatembezea kichapo na wawili hao kuomba msamaha, sungusunga hao waliachia na kuwaonya wasirudie tena kukutwa vichakani usiku.

VIMINI VYASABABISHA DIDA KUSHINDWA KUFANYA KAZI IKULU, SOMA ZAIDI HAPA



MTANGAZAJI wa Kipindi cha Mitikisiko ya Pwani kinachorushwa kupitia Radio Times, Hadija Shaibu ‘Dida’ amefunguka kuwa kamwe hawezi kufanya kazi Ikulu kutokana na vimini anavyovitinga.


Mtangazaji wa Kipindi cha Mitikisiko ya Pwani wa Radio Times, Hadija Shaibu ‘Dida’.

Akizungumza na Amani, Dida, alisema kuwa anafurahia sana kazi anayofanya kwa sababu inamruhusu kuvaa nguo yoyote anayojisikia vikiwemo vimini.
“Kufanya kazi Ikulu ningeshindwa kwani kuvaa nguo ni kwa sheria, huwezi kujivalia tu, kazi yangu nipo huru naweza kuvaa kitu chochote kile nikajisikia nina amani, lakini Ikulu lazima utinge koti na kuchomekea,” alisema Dida.

VIDONDA VYA TUMBO VINAVYOWATESA WENGI BILA KUJUA! SOMA HAPA KUJIJUA


Vidonda vya tumbo ni ugonjwa unaowasumbua watu wengi,  wanaume na wanawake na hata watoto wadogo. Tatizo hili husumbua sana na kumfanya mgonjwa asiweze kumudu shughuli zake za kila siku.
Ugonjwa huu huathiri kwa ujumla katika suala zima la afya.
Tatizo hili huanza taratibu na dalili za awali huwa hazionyeshi kama mtu ana ugonjwa huu.

Chanzo cha ugonjwa
Ugonjwa huu hutokana zaidi na maambukizi ya bakteria waitwao ‘Herictobacter Pylori’ au maarufu kama H. Pylori  hushambulia tabaka la ndani la tumbo.

Aina hii ya bakteria ni wagumu kufa kwa kuwa wana uwezo wa kuishi kwenye  mazingira ya tindikali tumboni. Tumboni kuna tindikali ya Hydrochloric Acid ambayo husaidia katika mmeng’enyo wa chakula.
Bakteria hawa wanaposhambulia tabaka la ndani la kizazi, hutegemea vishimo vishimo ambavyo ni vidonda hivyo tindikali inapotoka huchoma kwenye hivyo vidonda na kumfanya mgonjwa ahisi maumivu makali.

Aina za vidonda vya tumbo
Vidonda vya tumbo vipo vya aina mbili, kwanza ni vile vilivyopo mwanzoni mwa tumbo la chakula, Gastric Ulcers na ya pili ni Duodenal Ulcers katika sehemu ya pili ya tumbo. Maumivu na dalili za aina hizi mbili hufanana sana.

Ili kutofautisha aina hizi za vidonda, vipimo maalum hufanyika kama vile ‘OGD” na “Barium Meal’, vipimo ambavyo hufanyika katika hospitali za rufaa.
Dalili za ugonjwa
Hapa tutazungumzia dalili kuu za vidonda vya tumbo kwa ujumla. Mgonjwa wa vidonda vya tumbo katika hatua za awali huwa hajigundui kama ana tatizo.

Mgonjwa hulalamika kuhisi homa za mara kwa mara na kujihisi kama ana malaria au homa ya tumbo ‘Taifoidi’, wengine hulalamika kutumia sana dawa za taifoidi lakini hakuna nafuu.
Mwili unanyong’onyea, maumivu ya viungo, kuhisi baridi kuumwa kichwa na tumbo kujaa gesi.
Mgonjwa pia hulalamika maumivu ya tumbo eneo la chembe ya moyo ambapo ni chini ya kifua na juu ya kitovu.

Maumivu ya muda mrefu husambaa tumbo lote na tumbo huunguruma mara kwa mara .
Maumivu ya chembe ya moyo yaani chini ya kifua na juu ya kitovu husambaa hadi kifuani na kuzunguka mpaka mgongoni.

Mgonjwa hulalamika kuhisi moto kifuani na maumivu yaani kiungulia. Akilala usiku hali ya moto huongezeka na mgonjwa akicheua hutoa majimaji ya moto na machungu.
Mgonjwa hupata choo kigumu na vipande vipande kama cha mbuzi na wakati mwingine huwa cheusi.
Mgonjwa hupoteza hamu ya kula na wakati mwingine hutapika damu. Macho hupoteza nguvu ya kuona kwa kuwa muda wote anakuwa na maumivu, mwili unachoka na anakosa raha kutokana na kuwaza sana juu ya maumivu anayopata kiasi cha kumfanya mgonjwa akonde.

Mkojo unakuwa wa njano sana, hufunga kupata choo kikubwa na kusababisha maumivu ya kiuno kwa ndani ambayo husambaa hadi miguuni. Hamu ya tendo la ndoa pia hupotea.
Uchunguzi wa ugonjwa
Uchunguzi wa awali hufanyika katika vituo vya afya na hospitali za wilaya, mikoa na rufaa. Ni ugonjwa unaotibika hospitali na  vipimo ni kama Ultrasound, OGD, Barium Meal na vipimo vya damu ili kuangalia maambukizi ya H. Pylori na wingi wa damu.

Choo kikubwa pia kitapimwa. Ni muhimu pia kuangalia matatizo mengine kwa undani. Kipimo cha OGD ambacho kitapitishwa katika mfumo wa chakula kitasaidia kutoa majimaji yatakayopimwa maabara.
Ushauri
Ni vema mgonjwa azingatie kuhudhuria hospitali kwani ugonjwa wa vidonda vya tumbo huchunguzwa na kutibiwa hospitali ingawa tiba huchukua muda mrefu.

Ugonjwa huu dalili zake zinafanana sana na saratani au kansa ya tumbo hivyo ni vizuri uwahi hospitali ili ugundulike mapema.Unaweza ukawa unatumia dawa nyingine pasipo uchunguzi wa kidaktari mwishowe ukajikuta tayari hali inakuwa mbaya na kusababisha utumbo kutoboka au kansa.

KIJANA ANASWA LAIVU KWA KUUNDA MTAMBO WA KUWAIBIA AZAM, ZUKU,DSTV

Katika hali ya kushangaza, mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Ali, mkazi wa Mwananyamala jijini Dar, amekamatwa na polisi baada ya kudaiwa kuunganisha visivyo halali, mitambo ambayo iliwawezesha watu kuangalia matangazo ya televisheni ya vituo mbalimbali kwa malipo rahisi.
Bw. Ali anayedaiwa kuunganisha visivyo halali, mitambo ya kurusha matangazo ya televisheni ya vituo mbalimbali kwa malipo rahisi.
Awali, msamaria mwema mmoja alipiga simu kwa kikosi kazi cha Operesheni Fichua Maovu (OFM) cha Global Publishers na kukitonya juu ya uwezo wa mtu huyo anayewashangaza kwa utaalamu wake wa kuunganisha mitambo hiyo bila kugundulika.
Baadhi ya ving'amuzi vilivyokuwa vikitumiwa na mtuhumiwa kuunda mtambo wa mawasiliano.
“Hapa kuna watu kama 80 hivi wameunganishwa, wanaangalia televisheni za Azam, Zuku na nyingine kwa bei chee, lakini wanaangalia mipira, filamu na kila kitu, yaani huwezi kuamini kaka,” chanzo hicho kilinyetisha kwa OFM.
Bw. Ali (kushoto) akibanwa kwa maswali juu ya biashara haramu anayofanya.
Katika kujiridhisha, kikosi kazi chini ya kamanda mkuu, kilitembelea eneo la tukio na kufanya ukaguzi wa siri, uliothibitisha kuwepo kwa huduma hiyo, lakini bila ya kuwepo kwa dekoda za vituo hivyo vya televisheni vinavyotolewa kwa malipo.
Ulinzi mkali ukiimarishwa nje ya nyumba ya Bw. Ali.
Baada ya kujiridhisha huko, OFM ilifanya mawasiliano na wahusika wa vituo hivyo, ambao nao walitembelea eneo hilo la tukio na kujionea wenyewe. Wahusika hao walikuwa ni Afisa Leseni wa DSTV na Afisa Mauzo wa Azam Tv pamoja na mtu mmoja kutoka chama cha hakimiliki cha COSOTA.
Afisa Leseni kutoka chama cha hakimiliki COSOTA, Zephania Lyamuya (kulia) akisimamia zoezi.
OFM iliwashauri maofisa hao kuripoti jambo hilo kituo cha polisi, ushauri ambao waliukubali na kwenda kutoa taarifa Kituo cha Polisi Oystebay ambao waliongozana na watu hao hadi Mwananyamala.
Madishi ya Satelaiti yanayotumiwa na Bw. Ali kurushia matangazo ya televishen yakiwa juu ya nyumba yake.
Kufika nyumbani kwa mtuhumiwa huyo ambaye pia ni maarufu kwa jina la utani kama Masetelaiti, Polisi walifanikiwa kumkamata na baada ya upekuzi, waligundua kuwepo kwa mitambo ya aina mbalimbali, vikiwemo ving’amuzi vya aina mbalimbali, modulators, Receivers na vifaa vingine vikionekana vikiwa vimeunganishwa kwa utaalamu wa hali ya juu katika ukuta wa sebule yake.
Afisa Mkuu wa Mauzo kutoka kampuni ya Azam, Shah Seffu akiwa nje ya ofisi ya Bw. Ali.
Masetelaiti alikiri kuendesha maisha kwa staili hiyo na kudai kuwa utaalamu wa kuunganisha ving’amuzi hivyo ni wake mwenyewe na amekuwa akifanya hivyo kwa muda mrefu.
Afisa Leseni kutoka Cosota, Zephania Lyamuya alisema jamaa huyo anastahili kupelekwa Polisi kutoa maelezo kwani licha ya kutokuwa na leseni ya kufanya biashara hiyo, pia amekuwa akiwanyonya waigizaji wanaostahili kulipwa kila filamu zao zinaporushwa katika televisheni za nje.
Kikosi kazi kikifungua mitambo na kuharibu kazi haramu ya Bw. Ali.
Naye Afisa Mkuu wa Mauzo kutoka kampuni ya Azam aliyejitambulisha kwa jina la Shah Seffu (pichani kulia), alisema kuwa operesheni hiyo ni moja kati ya hatua walizozipanga kumaliza tatizo la kuingilia mawasiliano ya televisheni jambo ambalo limeonekana kukua kwa kasi nchini.
Baadhi ya Ving'amuzi vilivyokusanywa kutoka katika mtambo uliosukwa na Masatelaiti.
Baada ya kuvikusanya vifaa hivyo vilipelekwa katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay sambamba na mtuhumiwa kutoa maelezo ambapo jalada lilifunguliwa OB/RB/16106/2014, KUINGILIA MAWASILIANO YA TELEVISHENI

LAANA YA KANUMBA YAIMALIZA BONGO MUVI, ISOME HAPA

IMEVUJA! Kuvunjika kwa Kundi la Bongo Movie Unity kumedaiwa kuwa ni laana ya aliyekuwa memba hai wa kundi hilo, marehemu Steven Kanumba kutokana na kumnyanyapaa enzi za uhai wake, Ijumaa linakupa mchapo kamili.
Marehemu Kanumba.
TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini, Kanumba alikuwa ni miongoni mwa waasisi wa kundi hilo lakini kabla hajafa, yaliibuka majungu ambayo yalimsababisha ajiengue na kususia kundi hilo huku akiwa na kinyongo moyoni.

Wakilia juu ya kaburi la marehemu Kanumba.
“Kanumba hakufurahishwa na majungu yaliyokuwa yakiendelea ndani ya klabu dhidi yake, akajiapiza kwamba hatakaa akashiriki masuala ya kundi hilo hadi pale wahusika watakapojisafisha.
“Wakati sisi tukipanga yetu, Mungu naye anapanga yake. Kanumba alifariki wakati ambao wasanii waliomsukia majungu hayo hawajajisafisha, kama si kumuomba msamaha,” kilisema chanzo.

Staa wa filamu Bongo, Jackline Wolper.
KATIBU ASAKWA
Baada ya kunyaka maelezo hayo ya chanzo chetu, mapaparazi wetu walianza kuwatafuta waliokuwa viongozi wa klabu hiyo na kufanikiwa kumpata aliyekuwa katibu msaidizi, Devotha Mbaga, ambaye alikiri kwamba klabu hiyo ina laana ya Kanumba.

HUYU HAPA DEVOTHA
Akizungumza kwa hisia kali maeneo ya nyumbani kwake Kigamboni, jijini Dar, Devotha alisema mgogoro unaoendelea ndani ya kundi hilo ambalo linapumulia mashine baada mwenyekiti wao, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ na katibu wake, William Mtitu kujiuzulu ni laana ya Kanumba hivyo wanatakiwa kuomba radhi kaburini kwake.

Staa katika tasnia ya filamu Bongo,Wema Sepetu.
Alisema enzi za uhai wa Kanumba baadhi ya wasanii ambao wanagombana chini kwa chini kwa sasa ndani ya kundi hilo (majina yapo), walimnyanyapaa na walikuwa wakimchukia na kufikia hatua ya kuwakataza wanachama wote kutoshiriki kwenye filamu zake.
“Ukweli baadhi ya wasanii hasa hao viongozi wanatakiwa kutambua makosa waliyomfanyia Kanumba enzi za uhai wake na wamuomba msamaha kwani walimkosea sana na wakishaomba, naamini Bongo Movie itasimama lakini wasipofanya hivyo hiyo laana itaendelea kuwatesa na watapigana kila siku.
“Yaani kuna wakati hadi huwa nafikia hatua ya kusema bora Kanumba alikufa mapema yawezekana Mungu alikuwa na kusudi lake maana angeaibika na angeonekana ni mtu asiyefaa katika jamii kutokana na mikakati ambayo wasanii wenzake walikuwa wameipanga,” alisema Devotha.
Aliyekuwa mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Stive Mengere.
KUMBE WALIWAHI KUKAA KIKAO
Kama hiyo haitoshi, katika aya nyingine, Devotha alisema kuna wakati waliwahi kuweka kikao cha kusameheana kilichoandaliwa na Ridhiwan Kikwete ambaye sasa ni Mbunge wa Chalinze kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) lakini mambo bado yakawa ‘shagala baghala’.

“Nakumbuka kwenye kikao kimoja ambacho aliitisha Ridhiwan Kikwete kwa ajili ya wasanii na kusema kama kuna mtu amemkosea mwenzake wasameheane baada ya kuongea na sisi na kuondoka, watu walianza kuongea maneno mabaya ya kashfa na hapo ndipo walipopanga mikakati ya kumchafua na kutofanya kazi na Kanumba lakini baada ya siku chache alifariki.
Staa katika tasnia ya filamu Bongo, Vincent Kigosi 'Ray'.
“Hao wanaogombana sasa hivi ndiyo walikuwa vinara katika kumnyanyapaa Kanumba na ndiyo haohao siku ya mazishi yake ndiyo waliobeba jeneza, msalaba na kuvaa suti wakati walikuwa hawako naye vizuri, unajua roho huwa haifi kwa hiyo wanatakiwa kuomba msamaha ili wawe na amani,” alisema Devotha.
NI LAANA NZITO?
Kwenye mazungumzo hayo na waandishi wetu, Devotha aliendelea kutiririka kuwa kutokana Kanumba kufariki dunia akiwa na kitu moyoni kuna uwezekano mkubwa kwamba kuna kitu alikizungumza muda mchache kabla hajafariki au kuwa na kinyongo na Bongo Movie hivyo wasanii hao wanatakiwa kwenda kuomba msamaha kaburini kwake ili kundi hilo lisimame tena.

Staa katika tasnia ya filamu Bongo Dk. Cheni.
WAOMBA RADHI KIMYAKIMYA
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kwamba kuna baadhi ya wasanii wamedaiwa kuanza kwenda kaburini hapo kimyakimya na kuomba radhi ili kundi lao lirudi kwenye mstari kama lilivyokuwa enzi za marehemu Kanumba.

“Tumeona hali ni mbaya bora twende vinginevyo mambo yataharibika zaidi ya hapa,” alisema msanii mwenye taito kubwa ndani ya Bongo Movie kwa sharti la kustiriwa jina.
WENGINE KUOMBA RADHI
Ijumaa lilizungumza na baadhi ya wasanii kwa sharti la kutotaja majina yao ambao walikiri kwamba mambo hayaendi sawa kutokana na laana ya Kanumba hivyo wako mbioni kwenda kuomba msamaha katika kaburi lake wakiamini uliokufa ni mwili roho ingali hai.

KUMBUKUMBU
Marehemu Kanumba alifariki dunia Aprili 7, 2012 nyumbani kwake, Sinza-Vatcan akiwa na aliyekuwa mpenzi wake, Elizabeth Michael ‘Lulu’. Alizikwa katika Makaburi ya Kinondoni jijini Dar. 

DOKII AMPA ASKARI RUSHWA YA BUSU, MKASA MZIMA HUU HAPA

'Dokii' akitoa rushwa ya busu kumlainisha 'askari wa city'.
Mwigizaji wa kitambo na mwimbaji wa muziki wa Kizazi Kipya, Ummy Wenslaus 'Dokii' anadaiwa kutoa kali ya karne baada ya kumpa askari wa jiji rushwa ya busu, Ijumaa lina mkanda kamili.
Mwigizaji wa kitambo na mwimbaji wa muziki wa Kizazi Kipya, Ummy Wenslaus 'Dokii' akiomba ruksa ya kusepa na gari kutoka kwa askari wa jiji (city parking).
Tukio hilo ambalo gazeti hili lina picha za mnato na video lilijiri kwenye Makutano ya Mtaa wa Narung’ombe na Swahili, Kariakoo jijini Dar, asubuhi ya saa 4:00, Septemba 15, mwaka huu.
Kwa mujibu wa ‘shushushu’ wetu, Dokii alipaki ‘vibaya’ gari alilokuwa nalo aina ya Toyoya Noah la rangi nyeusi ambapo alifuatwa na kuambiwa kwamba sehemu aliyopaki hairuhusiwi.

Ilisemekana kwamba alitumia ‘ustaa’ wake kuwapuuza akaingia kwenye maduka na kuendelea na ‘shopping’ zake.Ilidaiwa kwamba aliporudi na kutaka kuondoka, alikuta mkoko huo umefungwa mnyororo na vyuma kwenye tairi la nyuma na askari wa jiji (city parking) hivyo akashindwa kutimua.
Ilielezwa kwamba baadaye alifuatwa na mkuu wa askari hao almaarufu kwa jina la Masai ambaye alimwambia kuwa alitakiwa kutoa faini ya shilingi elfu hamsini.
Iliendelea kudaiwa kwamba huku akidhani watu hawamjui alilianzisha na askari hao na kuanza kuzozana.
Muda mfupi baadaye ilijitokeza kadamnasi ambayo ilikuwa ikimzomea ndipo akakimbilia dukani kwa mwanaume aliyetajwa kwa jina moja la Chid.

'Dokii' akitoa namba ya simu kumlainisha askari huyo.
Ilidaiwa kwamba mwanaume huyo alimpatia msanii huyo shilingi elfu tano ili awapoze askari hao huku akimuombea wamfungulie gari aondoke lakini jamaa hao waliikataa.
Ilielezwa kwamba baada ya kuomba sana askari hao walikubali kumwachia baada ya kummwagia kiongozi wao mabusu ya kimahaba hadharani, kisa tu hakuwa na fedha ya kulipa faini.
Ilidaiwa kwamba baada ya kumlainisha jamaa huyo kwa mabusu motomoto na kufutiwa shitaka, aliachiwa huru bila kutoa chochote huku askari aliyeonjeshwa ‘utamu’ akibaki na mfadhaiko huku akiomba namba ya simu.
Askari wa 'city' akimruhusu 'Dokii' kuondoka eneo la tukio  mara baada kuchukua namba ya simu.
Ilisemekana kwamba ili kuua msala, msanii huyo alimpatia namba ya simu kisha akatoka nduki.
Ni rushwa? Kutoa kitu ili kununua haki kama alivyofanya Dokii ya kutoa busu ili aachiwe, nayo ni rushwa pia.Jitihada za kumpata Dokii ili kuzungumzia mkasa huo hazikuzaa matunda kufuatia simu yake ya kiganjani kuita bila kupokelewa hivyo jitihada zinaendelea. Stay tune!

AUNT EZEKIEL, HIVI KWELI WEWE NI MKE WA MTU, NA KWA NINI UNAPENDA WAUME ZA WATU?

NIMEWAHI kuzungumza mara kadhaa katika safu hii kuhusu huyu binti, mtoto wa nguli wa zamani wa soka Tanzania, Ezekiel Greyson ‘Jujuman’, aliyevuma sana akiwa na Simba. Anaitwa Aunt Ezekiel, staa wa filamu za Kibongo!
Nilisema kuwa katika tasnia ya filamu, ni muigizaji mzuri kwa kupamba sinema kutokana na uzuri wa sura na umbo lake, lakini katika wasanii wanaotakiwa kwa weledi na viwango, bado ni mtu wa kati, ingawa akiwa makini zaidi katika kazi yake, anaweza kuja juu!
Aunt, kama walivyo wasanii wenzake wenye majina, anavuma zaidi nje ya fani kuliko ndani. Wakati waigizaji kama Natasha, Aisha, Monalisa na Nora enzi zao walivuma kutokana na uwezo wao katika kazi wakiwa na makundi yao runingani, kizazi cha kina Aunt Ezekiel kinatikisa anga kikiwa katika kumbi za starehe na kwenye mikusanyiko ya watu!
Leo nazungumza tena na Aunt, hasa baada ya kujiuliza kwa muda mrefu na kushindwa kupata jibu, la kama muigizaji huyu yupo katika ndoa au alishaachika tena. Kumbukumbu zinaniambia aliwahi kuishi kwa kupika na kupakua na mtoto mmoja wa mjini, Jack Pemba na baadaye Hartman Mbilinyi kabla ya ndoa yake ya mwisho akiwa na Sunday Demonte.
Ingawa ni vigumu kuthibitisha, lakini ushahidi wa mazingira unaonyesha Aunt Ezekiel ni mmoja wa waigizaji wa kike ambao hawajatulia. Msanii huyu anadai yupo katika ndoa na mumewe Demonte, ambaye anaelea katika uvumi kwamba huko aliko, yupo matatizoni.
Ni kipindi kirefu tokea mumewe alipoondoka nchini kuelekea Ughaibuni. Sipendi sana kumuongelea yeye kwa sababu hayo ni masuala ya kibinafsi, lakini hili la Aunt linanipa ugumu kidogo kulikalia kimya.
Aunt anadaiwa kutoka kimapenzi na bwana mdogo mmoja mcheza shoo wa Diamond, anayeitwa Moses Iyobo. Mapenzi yao yalianza kwa siri, lakini wenyewe mara kadhaa kwa nyakati flani wamewahi kunukuliwa wakisema kuwa hawaachani ng’o!Iyobo anadaiwa pia kuwa na mke, ambaye aliwahi hata kuleta kasheshe kubwa baada ya kubaini uhusiano huo.
Ninajiuliza, Aunt ameolewa, shemeji na wifi zake wapo hapahapa mjini, inakuwaje anafanya mambo hadharani namna hii?Anyway, huenda basi hayo ni mambo ya familia, wanajuana wenyewe, lakini kwa jamii inayomtazama huyu binti, hasa watoto, anaifundisha nini kuhusu maisha ya ndoa?
Kwamba unaweza kumuacha mumeo Mwanza, ukaja Dar es Salaam na kutanua tu ovyo na waume wa wenzio? Huenda, kama ni kweli kwamba mumewe yupo matatizoni, kama binadamu anaweza kujikuta akiwa na mahitaji ya kimaumbile.
Kama ni hivyo, sasa kuna tatizo gani kufanya kwa siri? Watu kibao tu wanafanya michepuko nje ya ndoa, lakini si wanafanya kwa kujificha ili kulinda heshima ya familia zao?
Lipo tatizo la msingi ambalo linapaswa kurekebishwa na huyu dada haraka. Kama ametengana na mumewe, aweke hadharani ili kupunguza maswali haya, kwa vile mashabiki wake na wale wa fani yake kwa jumla, wajifunze nini kwake, kwamba unaweza kuolewa au kuoa na wakati huo huo ukawa huna hofu na penzi lingine?
Hapana, huu ni uhuni usiokubalika. Kuoa au kuolewa kunamaanisha ni mwisho wa maisha yako ya kutangatanga kingono, umeamua kutulia kwa mmoja umpendaye. Kama alikuwa bado hajatosheka kwa nini alijiongopea?
Jambo lingine la kumshauri ni kuwa umri unasogea, asije kujikuta anazeeka na ujana bado haujamwisha, kwa sababu kwa jinsi anavyoyaendesha maisha yake, ni kama vile nayo anaigiza kama anavyofanya kwenye filamu!