UPENDO! Shosti mkubwa wa marehemu Recho Haule,
Jennifer Kyaka ‘Odama’ amejitolea kujenga kaburi la rafiki yake huyo
aliyefariki mapema mwaka huu.
“Recho alikuwa ndiyo kila kitu kwangu, alikuwa msiri wangu. Hivyo nimeona ni vyema tukalistiri vizuri kaburi lake na kwa msaada wa Saguda, nashukuru Mungu tumefanikisha kwa kiasi fulani, tutaendelea kulijenga zaidi.”






